Asili na mazingiraTaiwan
Taiwan yakumbwa na mfululizo wa matetemeko ya ardhi
23 Aprili 2024![Taiwan | Vikosi vya uokoaji](https://static.dw.com/image/68727414_800.webp)
Matangazo
Mamlaka nchini humo hata hivyo zimesema hakukuwa na uharibifu mkubwa ulioshuhudiwa. Matetemeko zaidi yalisikika maeneo ya jimbo la Hualien na mji mkuu Taipei.
Soma zaidi:Mamia wahamishwa kutoka hifadhi ya taifa baada ya tetemeko Taiwan
Mnamo April 3 mwaka huu, watu 17 walikufa huko Taiwan kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lenye ukubwa wa 7.4 ambalo pia lilisababisha maporomoko ya udongo na uharibifu mkubwa wa majengo na miundombinu.