1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Wanafunzi 14 watekwa nyara na watu wenye silaha Nigeria

17 Aprili 2026

Watu wenye silaha wamewateka nyara wanafaunzi wasiopungua kumi na wanne waliokuwa wakielekea kwenye mitihani ya kujiunga na elimu ya chuo kikuu katika jimbo la Benue Kaskazini mwa Nigeria.

Wabeba silaha wamewateka nyara wanafunzi 14 nchini Nigeria
Mabegi ya wanafunzi waliowahi kutekwa nyara nchini Nigeria Desemba 16, 2026 yakiwa darasani Picha: Sunday Alamba/AP Photo/picture alliance

Kamishna wa polisi wa jimbo hilo Ifeanyi Emenari amesema vijana hao walitekwa nyara Alhamisi walipokuwa njiani wakisafiri kwa basi kuelekea katika mji wa Otukpo ambako mtihani wao ulipangwa kufanyika. Mamlaka za usalama nchini humo zimeanzisha msako wa kuwaokoa wanafunzi hao.

Wanamgambo waendelea kutishia usalama

Makundi ya wabeba silaha na wanamgambo wenye itikadi kali wamekuwa wakiwateka nyara wasafiri, wanafunzi na jamii za vijijini nchini Nigeria. Hadi sasa mamlaka hazijabaini waliohusika na hakuna kundi lolote lililokiri kuhusika na utekaji huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW