1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Takriban watu 18 wauawa kwenye shambulizi la RSF, Sudan

17 Septemba 2025

Takriban watu 18 waliuawa jana Jumanne wakati wa uvamizi uliofanywa na wanamgambo wa RSF katika mji uliozingirwa wa El- Fasher, jimbo la Darfur nchini Sudan. Haya ni kwa mujibu wa vyanzo viwili vya matibabu.

Wapiganaji wa RSF nchini Sudan washika doria kwenye eneol la mkutano wa kiongozi wao Jenerali Mohammed Hamdan Dagalo mnao Juni 22, 2019
Wapiganaji wa RSF nchini SudanPicha: Hussein Malla/AP Photo/picture alliance

Vyanzo hivyo pia vimesema idadi ya watu isiyojulikana wanaaminika kuzikwa hasa katika eneo la kusini la kambi ya wakimbizi ya Abu Shouk, viungani mwa mji huo.

Kundi moja la wanaharakati, moja kati ya mamia ya makundi yanayoorodhesha maasi yanayofanyika katika vita hivyo, limesema wapiganaji wa RSF wamekuwa wakisonga mbele tangu Jumatatu kutoka kaskazini mwa mji huo ambapo mashambulizi yanaendelea.

Kundi hilo limesema raia kadhaa waliuawa majumbani mwao na wengine kuwekwa kizuizini chini ya mazingira ya kutatanisha.

Pia limeripoti kutokea kwa mapigano makali, mashambulizi na kuendelea kuwepo kwa droni katika anga ya El-Fasher kwa siku ya pili mfululizo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW