Takriban watu 45 wameuawa katika mapigano Somalia
10 Juni 2024![Pressefreiheit Medienfreiheit in Afrika | Journalisten bei der Arbeit in Somalia](https://static.dw.com/image/60212636_800.webp)
Matangazo
Afisa wa polisi wa jimbo la Galgadud, Ahmed Sahal amesema tukio hilo baya limehusisha wapiganaji kutoka katika koo za Marehan na Dir.
Mzozo huo ulitokea kwenye mji wa Landhere huko kaskazini ya Galgadud.
Kihistoria raia wa Somalia kwa idadi yao wamegawanywa katika koo na mara nyingi hujihusisha na migogoroya maeneo kwa ajili ya rasilimali na sababu za kisiasa.