Watu milioni 4.4 kutoka Ukraine wana hadhi ya ulinzi Ulaya
11 Machi 2026
Matangazo
Ripoti iliyochapisha jana Jumanne inaonesha takwimu hiyo iliongezeka kwa 23,110, au asilimia 0.5 ikilinganishwa na mwisho wa mwezi Desemba 2025.
Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zinazohifadhi idadi kubwa zaidi ya wanufaika wa ulinzi wa muda kutoka Ukraineni Ujerumani yenye milioni 1.26, Poland yenye 956,990 na Jamhuri ya Czech yenye 397,185.
Wakimbizi wengi wa Ukraine wanaruhusiwa kufanya kazi katika nchi za Umoja wa Ulaya na pia kupokea fedha za kijamii na huduma za matibabu bila kulazimika kuomba hifadhi.
Umoja wa Ulaya umeongeza muda wa hatua hizi hadi Machi 2027, na mawaziri wa mambo ya ndani kwa sasa wanajadili kurefusha muda zaidi.