Tangazo la vizuizi bandari za Iran lapandisha bei za mafuta
13 Aprili 2026
Matangazo
Gharama ya pipa moja la mafuta ghafi ya Marekani imepanda kwa asilimia 8 na kufikia dola 104 huku katika soko la dunia pipa moja la mafuta linauzwa kwa dola 102 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.
Bei ya mafuta imeyumba mara kadhaa wakati wa vita vya Iran, ikipanda kutoka dola 70 kwa pipa kabla ya vita na kufikia hadi karibu dola 120.
Kabla ya kuanza mazungumzo kati ya Iran na Marekani nchini Pakistan, bei ya mafuta ilishuka kidogo kwenye soko la dunia kwa matumaini mwafaka ungepatikana na kuondoa vizuizi hasa kwenye Mlango Bahari wa Hormuz ambao sasa unadhibitiwa na Tehran.