TBILISI: Watu watatu wauwawa kwenye mripuko wa gesi
27 Oktoba 2006Matangazo
Watu watatu wameuwawa kwenye mripuko kwenye kituo cha gesi ya oxygen katika mji mkuu wa Georgia, Tbilisi. Watu wengine wawili wamejeruhiwa vibaya katika mripuko huo uliokiharibu kabisa kituo hicho.
Msemaji wa idara inayohusika na shughuli za uokozi amesema inahofiwa huenda maiti mbili au tatu zikawa zimefunikwa chini ya vifusi. Mripuko huo umeelezwa kuwa ajali.