Janga
Tetemeko la Ardhi Bangladesh lasababisha mauaji ya watu 4
21 Novemba 2025
Matangazo
Kwa mujibu wa Shirika la kuchunguza matetemeko ya ardhi la Marekanila USGS, tetemeko hilo lilipiga maeneo hayo na athari zake zilishuhudiwa katika eneo la Ghorashal huko Bangladesh.
Tetemeko hilo lililodumu kwa sekunde kadhaa liliyumbisha majengo kadhaa na kusababisha hofu miongoni mwa raia waliokimbilia barabarani.
Mashirika ya huduma ya zimamoto na mashirika ya dharura ya ulinzi wa raia yaliripoti kuwepo kwa nyufa kadhaa katika majengo mengi mjini Dhaka.
Mtoto wa miezi 10 ni miongoni mwa waliouwawa wakati kuta ya nyumba yao ilipomuangukia.