1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaChina

Tetemeko la ardhi la ukubwa wa 7.1 lapiga eneo la Xinjiang

23 Januari 2024

Tetemeko la ardhi la ukubwa wa 7.1 katika kipimo cha Ritcha limepiga eneo la mpaka wa Kyrgyzstan-Xinjiang huku kukiwa na ripoti za majeruhi kadhaa na nyumba kuanguka.

Athari za tetemeko la ardhi mjini jijini Wajima, katikati mwa Japan.
Athari za tetemeko la ardhi mjini jijini Wajima, katikati mwa Japan.Picha: Taketo Osihi/Yomiuri Shimbun/AP/picture alliance

Kulingana na idara ya hali ya hewa ya China, tetemeko hilo limetokea majira ya saa nane usiku wa kuamkia leo na limepiga karibu na mkoa wa Xinjiang kaskazini magharibi mwa China.

Shirika la habari la serikali Xinhua limeripoti kuwa, kampuni ya reli imesitisha mara moja safari zake huku treni 27 zikiathirika na tetemeko hilo la ardhi.

Mamlaka ya kukabiliana na majanga imesema tayari imetuma timu ya uokoaji katika eneo la mkasa.

Katika muda wa saa 24 zilizopita, mkoa wa Xinjiang na viunga vyake umekumbwa na matetemeko kadhaa ya ardhi.

Nchi jirani ya Kazakhstan, idara zinazohusika na kukabiliana na majanga zimeripoti tetetemo la ardhi la ukubwa wa 6.7. 

Mitetemeko mengine ya ardhi imeripotiwa pia nchini Uzbekistan.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW