Migogoro
Thailand yafikiria kusitisha kuiuzia mafuta Cambodia
14 Desemba 2025
Matangazo
Msaidizi wa msemaji wa jeshi la wanamaji la Thailand Kepteni Nara Khunkothom, ameeleza kuwa Makamanda wa jeshi la nchi hiyo wamelitaka pia jeshi la wanamaji kuwa makini dhidi ya meli zinazobeba bidhaa muhimu za kimkakati.
Maeneo ya Bahari karibu na bandari za Cambodia kutangazwa kuwa ya hatari
Wamejadili pia juu ya uhitaji wa kuyatangaza maeneo ya Bahari karibu na bandari za Cambodia kuwa "ya hatari kubwa”. Thailand inafikiria kuchukua hatua hiyo saa kadhaa baada ya kutangaza amri ya kutokutoka nje katika mkoa wake wa kusini mashariki wa Trat wakati mzozo kati ya nchi hizo na Asia ukipamba moto.