1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Timu 16 zajikatia tikiti ya hatua ya mchujo

10 Desemba 2015

Michuano ya Klabu bingwa Ulaya – UEFA Champions League zimeingia sasa katika hatua ya mchujo baada ya timu 16 kujikatia tikiti katika mechi za mwisho za makundi

UEFA Champions League Bayer 04 Leverkusen vs. FC Barcelona
Picha: Getty Images/AFP/P. Stollarz

Katika mechi za kundi D, Bayer Leverkusen iligawana pointi na Barcelona kufuatia sare ya bao 1–1, Olympiakos wakiwa nyumbani dhidi ya Arsenal wakaambulia kichapo cha mabao 3-0 yaliyofungwa yote na Mfaransa Olivier Girioud.

Chelsea wakiwa katika ngome ya Stamford Bridge walijikatia tikiti kwa ushindi wa mabao 2 – 0 dhidi ya FC Porto, Valencia chini ya uongozi wa kocha mpya Garry Neville imechapwa bao 2 - 0 na Lyon,

FC Roma ilitoshana nguvu na BATE Borislov kwa kutoka sare ya kutofungana bao wakati miamba ya Ujerumani, Bayern Munich ikiichapa Dinamo Zagreb bao 2-0. Dynamo Kiev iliwafunga Macabbi Tel-Aviv bao 1–0 na KAA Gent ya Ubelgiji ikafunga kazi kwa kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Zenit ya Urusi.

Orodha kamili ya timu zilizofuzu katika hatua ya mchujo ya UEFA Champions League:

Timu zilizokuwa kileleni kwenye Makundi: Real Madrid, Wolfsburg, Atleico Madrid, Man City, Barcelona, Bayern Munich, Chelsea, Zenit

Timu zilizomaliza katika nafasi ya pili kwenye makundi: PSG, PSV, Benfica, Juventus, Roma, Arsenal, Dynamo Kiev, Gent.

Droo ya raundi ya muondowano ya timu 16 itafanyika Jumatatu Desemba 14.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW