1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump afikiria kumaliza vita vyake Mashariki ya Kati

21 Machi 2026

Rais wa Marekani Donald Trump amesema utawala wake unafikiria kumaliza operesheni za kijeshi Mashariki ya Kati licha ya nchi hiyo kutangaza kutuma meli zaidi za kivita na jeshi la wanamaji katika eneo hilo.

USA Washington D.C. 2025 | Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Nathan Howard/REUTERS

Taarifa hizo za mkanganyiko za Marekani zinakuja baada ya kupanda tena kwa bei ya mafuta na hivyo kupelekea kushuka kwa soko la hisa la Marekani. Hayo yanafuatiwa pia na tangazo la utawala wa Trump kwamba utaondoa vikwazo dhidi ya mafuta ya Iran yanayopakiwa kwenye meli, hatua inayolenga kukabiliana na ongezeko hilo la bei ya mafuta.

Hata hivyo, vita hivyo havijaonyesha dalili za kupungua licha ya Iran kusherehekea hii leo sikukuu ya Eid el Fitr.

Israel imesema Iran imeendelea kufyatua makombora mapema leo Jumamosi, huku Saudi Arabia ikisema imedungua droni 20 ndani ya saa kadhaa katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo, ambalo ni makazi ya mitambo mikubwa ya mafuta.

Wizara ya ulinzi ya nchi hiyo imesema hakukuwa na majeruhi wala uharibifu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW