1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump aikosoa jumuiya ya kujihami ya NATO kuhusu Iran

9 Aprili 2026

Rais wa Marekani Donald Trump ameikosoa jumuiya ya kujihami ya NATO kuhusiana na vita vya Iran wakati alipokutana na katibu mkuu wa jumuiya hiyo, Mark Rutte mjini Washington.

Rais Donald Trump. kulia, ameikosoa jumuiya ya NATO kwa kutoisaidia Marekani katika vita vyake dhidi ya Iran.
Rais Donald Trump. kulia, ameikosoa jumuiya ya NATO kwa kutoisaidia Marekani katika vita vyake dhidi ya Iran.Picha: Evan Vucci/AP Photo/picture alliance

Trump alisema amevunjwa moyo na kukatishwa tamaa kwa kuwa NATO haikuwepo wakati Marekani na Israel zilipoanzisha mashambulizi dhidi ya Iran.

Lakini Rutte kwa upande wake alisema alifanikiwa kuashiria ukweli kwamba idadi kubwa ya mataifa ya Ulaya yamekuwa yakisaidia katika kuweka kambi za kijeshi, uratibu na mipangilio, kwa kutumia ndege za ziada, na kuhakikisha yanatimiza ahadi zao.

Rutte alifanya mkutano wa faraghani na Trump kwa ajili ya majadiliano ambayo yalitarajiwa kuzingatia kuufungua tena mlango bahari wa Hormuz na kutuliza hasira ya Trump dhidi ya NATO kuhusu vita vya Iran.

Ikulu ya Marekani ilisema Trump angejadili uwezekano wa kuondoka katika muungano huo baada ya kushindwa kujiunga na vita hivyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW