1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMarekani

Trump ajiunga na mtandao wa TikTok

Saleh Mwanamilongo
2 Juni 2024

Trump alitishia kupiga marufuku mtandao huo wa video fupi unaomilikiwa na kampuni kubwa ya China ya kiteknolojia ya ByteDance, alipokuwa rais kabla ya uchaguzi wa Novemba 2020.

Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump ajiunga na mtandao wa TikTok, licha ya kutaka kuupiga marufuku
Rais wa zamani wa Marekani Donald Trump ajiunga na mtandao wa TikTok, licha ya kutaka kuupiga marufukuPicha: Jakub Porzycki/NurPhoto/picture-alliance

Gazeti la Politico, ambalo iliripoti habari hiyo kwa mara ya kwanza, limesema Trump alichapisha video ya uzinduzi kwenye akaunti yake ya TikTok Jumamosi usiku. Video ilionyesha Trump akiwasalimia mashabiki kwenye mpambano wa mchezo wa mieleka wa Ultimate Fighting huko New Jersey.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW