1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Trump amsamehe Giuliani na wapambe wengine

10 Novemba 2025

Rais Donald Trump amewasamehea wapambe wake walioshutumiwa kushiriki jaribio la kubatilisha ushindi wa uchaguzi wa 2020.

USA New York 2025 | Rudy Giuliani vor dem Bundesgericht in Manhattan
Picha: Ted Shaffrey/AP Photo/picture alliance

Kulingana na afisa mkuu wa kitengo hicho cha msamaha wa rais, Ed Martin, miongoni mwa wale ambao Donald Trump amewasamehe ni waliokuwa mawakili wake Rudy Giuliani na Sidney Powell na pia aliyekuwa afisa mwandamizi Mark Meadows ambao wamepewa msamaha bila masharti yoyote.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Martin amechapisha orodha ya watu 70 ambao wamesamehewa.

Majina yaliyo kwenye orodha yalihusishwa katika mpango wa kubadilisha orodha za wapiga kura katika majimbo ya ushindani mkali, yakiwemo Arizona, Georgia na Michigan, ambayo Joe Biden alikuwa amepata kura nyingi katika uchaguzi wa urais ya mwaka 2020

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW