SiasaMarekani
Trump amsamehe Giuliani na wapambe wengine
10 Novemba 2025
Matangazo
Kulingana na afisa mkuu wa kitengo hicho cha msamaha wa rais, Ed Martin, miongoni mwa wale ambao Donald Trump amewasamehe ni waliokuwa mawakili wake Rudy Giuliani na Sidney Powell na pia aliyekuwa afisa mwandamizi Mark Meadows ambao wamepewa msamaha bila masharti yoyote.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Martin amechapisha orodha ya watu 70 ambao wamesamehewa.
Majina yaliyo kwenye orodha yalihusishwa katika mpango wa kubadilisha orodha za wapiga kura katika majimbo ya ushindani mkali, yakiwemo Arizona, Georgia na Michigan, ambayo Joe Biden alikuwa amepata kura nyingi katika uchaguzi wa urais ya mwaka 2020