Trump anaanza ziara ya kitaifa nchini Uingereza
17 Septemba 2025
Matangazo
Trump aliyewasili Uingereza Jumanne jioni akifuatana na mkewe Melania, atakaribishwa na Mfalme Charles III kwenye kasri la Windsor kwa halfa ya fahari itakayojumuisha heshima ya zulia jekundu, gwaride la kijeshi na dhifa ya chakula cha jioni.
Kwa desturi, Uingereza huwakaribisha viongozi wa kigeni kufanya ziara moja pekee ya kitaifa na Trump alipata heshima hiyo mwaka 2019 alipoalikwa kuitembelea Uingereza na Malkia Elizabeth II.
Hata hivyo ziara hii nyingine ambayo si ya kawaida inazingatiwa kuwa sehemu ya mkakati wa Uingereza wa kumweka karibu kiongozi huyo anayejulikana kwa sera zisizotabirika.