Trump aonya Israel kutoingilia masuala ya Syria
2 Desemba 2025
Matangazo
Kupitia mtandao wake wa kijamii Truth Social, Rais Trump ameandika "Ni muhimu sana Israel kudumisha mazungumzo madhubuti na ya kweli na Syria, na kuhakikisha hakuna kinachofanyika kitakachozuia mabadiliko ya Syria kuwa taifa lenye ustawi." Trump amekuwa akisisitiza juu ya makubaliano ya usalama kati ya Israel na Syria tangu kuangushwa kwa mtawala wa muda mrefu Bashar al-Assad mwaka mmoja uliopita. Hata hivyo, mvutano umeongezeka kutokana na mamia ya mashambulizi ya Israel dhidi ya Syria. Katika shambulio la kifo vingi hadi sasa, vikosi vya Israel viliua watu 13 Ijumaa katika operesheni kusini mwa Syria, wakisema walilenga kundi la Kiislamu.