Trump: Lebanon si sehemu ya makubalino ya kusitisha vita
9 Aprili 2026
Kauli ya Trumo imekuja huku Israel ikifanya wimbi kubwa la mashambulizi dhidi ya Lebanon baada ya makubaliano hayo kutangazwa. Iran kwa upande wake imesema itakomesha usitishaji mapigano kwa upande mmoja ikiwa mashambulizi ya Israel yataendelea dhidi ya Lebanon.
Wizara ya afya ya Lebanon imetangaza idadi ya vifo kutokana na mashambulizi makubwa ya Israeli jana Jumatano kuwa watu 182.
Kamati ya kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) ilisema imekasirishwa na vifo na uharibifu huo mbaya. Kundi la Hezbollah limesema hivi leo limevurumisha maroketi kuelekea kaszini mwa Israel kujibu mashambulizi hayo.
Wakati haya yakiarifiwa, waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Israel iko tayari kurudi vitani baada ya kutangazwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano na Iran.