Trump ataka mateka wanaoshikiliwa Gaza waachiwe huru
24 Septemba 2025
Matangazo
Akihutubia Jumanne katika mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Trump amesema nchi zenye nguvu duniani zinapaswa kuangazia juhudi za kuhakikisha mateka wanaoshikiliwa Gaza wanaachiwa huru.
Trump amezungumzia pia vita vya Urusi nchini Ukraine, mabadiliko ya tabianchi, na uhamiaji haramu.
Viongozi wengine waliohutubia Jumanne katika Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa ni pamoja na Rais wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Rais wa Korea Kusini Lee Jae Myung, Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa, na Mfalme Abdullah II wa Jordan.
Viongozi hao kwa nyakati tofauti walizungumzia kuhusu matumizi ya silaha, mizozo ya kimataifa, kuongeza misaada ya maendeleo, na kupunguza madeni kwa nchi maskini zaidi.