1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump ataka Netanyahu apewe msamaha wa rais

12 Novemba 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amemtaka Rais wa Israel Isaac Herzog kumpa msamaha wa rais Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kutokana na kesi za ufisadi zinazomkabili.

Israel Jerusalem 2025 | Donald Trump und Benjamin Netanjahu in der Knesset
Picha: Evan Vucci/REUTERS

Kulingana na ofisi ya Herzog, Trump ametuma barua kwa Herzog leo akisema kesi dhidi ya Netanyahu ambaye kwa pamoja wamekuwa wakipambana na Iran, ni kesi iliyochochewa kisiasa.

Ofisi hiyo ya rais wa Israel lakini imesema mtu yeyote anayetaka msamaha wa rais ni sharti awasilishe ombi rasmi kwa mujibu wa mwongozo uliopo.

Tump alipofanya ziara Israel mwezi uliopita wa Oktoba, alitoa wito kama huo kwa Herzog. Netanyahu na mkewe Sara katika mojawapo ya kesi hizo wanatuhumiwa kupokea vitu vya thamani ya zaidi ya dola 260,000 kutoka kwa mabilionea waliotaka kufanyiwa hisani za kisiasa.

Katika kesi nyengine mbili, waziri mkuu huyo wa Israel pia anatuhumiwa kujaribu kuvishawishi vyombo viwili vya habari nchini Israel kutoripoti habari mbaya kumhusu.

Netanyahu anakanusha mashtaka hayo na amesema kuwa hana hatia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW