1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Trump awalaumu "mrengo wa kushoto" mauaji ya Kirk

11 Septemba 2025

Rais Donald Trump wa Marekani ameapa kuwasaka na kuwatia nguvuni waliohusika na mauaji ya mmoja wa wafuasi na wapiga debe wake wakubwa, Charlie Kirk, akiwatuhumu wanasiasa wa "mrengo mkali wa kushoto" kwa mauaji hayo.

Charlie Kirk
Charlie Kirk, mpiga debe wa Donald Trump aliyepigwa risasi na kuuawa siku ya Jumatano (Septemba 10, 2025).Picha: Cheney Orr/REUTERS

Trump aliandika kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social kwamba wanasiasa wa mrengo mkali wa kushoto "wamekuwa wakiwalinganisha Wamarekani wazuri kama Charlie na Manazi na ndio chanzo cha mauaji na ugaidi ndani ya nchi."

Kirk, ambaye alikuwa muasisi na kiongozi mwenza wa kundi la vijana lililosaidia kampeni ya kumrejesha madarakani  Trump,  alipigwa risasi na kuuawa siku ya Jumatano (Septemba 10) akiwa kwenye mkutano katika Chuo Kikuu cha Uttah Valley.

Picha ya video inamuonesha Kirk akianguka jukwaani alipokuwa akizungumza baada ya mlio wa risasi kusikika.

Wapelelezi wanaamini hayo yalikuwa mauaji ya kupanga na kwamba muuaji alikuwa amekaa kwenye paa la chuo hicho. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW