Trump kukutana na kiongozi wa upinzani wa Venezuela
13 Januari 2026
Afisa wa serikali ya Marekani ameliambia shirika la habari la AFP kwamba mkutano huo utafanyika siku ya Alhamisi katika Ikulu ya White House.
Machado amekuwa akitengwa na Washington tangu majeshi ya Marekani yalipomkamata kiongozi wa muda mrefu Nicolas Maduro tarehe 3 Januari, hatua iliyofuatwa na utawala wa Trump kutangaza kuisimamia Venezuela.
Kwa kumwacha pembeni Machado na mshirika wake Edmundo Gonzalez Urrutia, Trump amekuwa akifanya kazi na rais wa muda Delcy Rodriguez, aliyeachwa madarakani pamoja na washirika wa karibu wa Maduro.
Trump amemwonya Rodriguez kufuata maelekezo ya Marekani — hasa kuhusu kuruhusu upatikanaji wa akiba kubwa ya mafuta ya nchi hiyo ya Amerika Kusini.
Wakati huohuo, Venezuela imetangaza kuwaachilia huru watu wengine 116 waliokuwa wamefungwa chini ya utawala wa Maduro — wengi wao kwa kushiriki maandamano baada ya uchaguzi wa mwaka 2024 uliogubikwa na utata.