1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump, Starmer wasaini mikataba mikubwa ya uwekezaji

18 Septemba 2025

Ziara ya pili ya kihistoria ya Rais wa Marekani Donald Trump nchini Uingereza imehitimishwa leo Alhamisi kwa mazungumzo na Waziri Mkuu Keir Starmer.

 Aylesbury 2025 | Donald Trump Keir Starmer
Uingereza na Marekani wasaini mikataba mikubwa ya uwekezaji katika teknolojia na nishati ya nyuklia.Picha: Andrew Caballero-Reynolds/AFP/Getty Images

Viongozi hao wawili wamesaini mkataba mkubwa wa uwekezaji katika teknolojia, ikiwemo akili bandia na nishati ya nyuklia, mkataba ambao unatarajiwa kuleta maelfu ya ajira na mabilioni ya fedha za uwekezaji.

Hapo jana, Trump na mkewe Melania walipokelewa kwa heshima kubwa na Mfalme Charles wa Tatu na Malkia Camilla katika kasri la Windsor, ikiwa ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani au kiongozi yeyote wa dunia kualikwa kwa mara ya pili katika ziara ya kiserikali.

Waziri Mkuu Starmer alisisitiza urafiki na heshima ya kweli kati yake na Trump, akisema ni heshima kumkaribisha kiongozi huyo wa Marekani aliyemuita rafiki yake.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW