1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Janga

"Tupo pamoja nanyi" Klöckner, aliambia bunge la Ukraine

11 Machi 2026

Spika wa bunge la Ujerumani Julia Klöckner, amewahakikishia raia wa Ukraine kwamba Ujerumani inaendelea kuwa pamoja nao wakati ikiendelea kupambana na uvamizi wa Urusi.

Ukraine Kiev | Julia Klöckner
Spika wa bunge la Ujerumani Julia KlöcknerPicha: Mykola Berdnyk/DW

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kwanza  katika taifa hilo linalokumbwa na vita.

Akiwa mwakilishi wa kwanza wa Ujerumani kulihutubia bunge la Ukraine, Klöckner aliwaambia wabunge kwamba Ujerumani siku zote ipo upande wao.

Julia Klöckner aliwasili mjini Kiev kwa usafiri wa treni na ziara yake haikutangazwa kutokana na sababu za kiusalama. Alipokewa na mwenyekiti wa bunge la nchi hiyo Ruslan Stefanchuk, na hapo baadaye atakutana na rais Volodymyr Zelensky.

Klöckner pia alitembelea kituo cha nishati ya umeme, ili kuona athari iliyosababishwa na mashambulizi ya Urusi nchini humo yaliyolenga miundombinu ya nishati na kuwaacha wakaazi wengi katika baridi kali kipindi hiki cha majira ya baridi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW