1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Turk: Vita mjini El- Fasher ni doa kwa jamii ya kimataifa

14 Novemba 2025

UN imesema leo kuwa mauaji ya kutisha katika mji wa El-Fasher nchini Sudan ni "doa" kwa ulimwengu, na ikaitaka jamii ya kimataifa kuchukua hatua kufuatia onyo la uhalifu dhidi ya ubinadamu na mauaji ya halaiki.

Kamishna Mkuu wa Haki za Binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk 
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk Picha: Uncredited/AP/dpa/picture alliance

Akifungua kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu El-Fasher, Kamishna Mkuu wa Haki za Binaadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk  amesema jamii ya kimataifa haijaingilia kati licha ya ripoti za mara kwa mara za "ukatili wa kutisha" na kuwaonya wahusika kuwa watawajibishwa.

Turk ameonya kuwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu imeashiria kuwa inafuatilia hali hiyo kwa karibu.

''Wote waliohusika katika mzozo huu wanapaswa kujua. Tunawatazama na haki lazima itendeke. Sudan imejikuta katika vita vya uwakilishi wa raslimali asili na mali zake. Nchi nyingi katika eneo hilo na kwingineko zinahusika.''

Rasimu ya azimio inayojadiliwa leo Ijumaa inalaani aina zote za uingiliaji kutoka nje unaochochea mzozo huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW