1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UAE yakaribisha mpango wa amani wa Marekani kwa Sudan

9 Februari 2026

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa UAE amesema wameukaribisha mpango kamili wa Amani kwa Sudan uliotangazwa na mshauri mkuu wa Marekani wa Masuala yanayohusu nchi za Kiarabu na Afrika Massad Boulos.

Sudan I  Abdel Fattah al-Burhan
Kiongozi wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-BurhanPicha: Stringer/Anadolu Agency/IMAGO

Umoja wa Falme za Kiarabu umethibitisha hapo jana kuukaribisha mpango wa amani unaoungwa mkono na Marekani kwa ajili ya vita nchini Sudan, ambapo nchi hiyo ya Ghuba imekuwa ikishutumiwa mara kadhaa kuuchochea mzozo huo.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa  UAE ameandika katika mtandao wa kijamii wa X kwamba nchi hiyo imeukaribisha mpango kamili wa Amani kwa Sudan uliotangazwa na mshauri mkuu wa Marekani wa Masuala yanayohusu nchi za Kiarabu na Afrika Massad Boulos.

Tangu Aprili 2023, vita kati ya jeshi la Sudan na kikosi cha wanamgambo wa RSF vimesababisha vifo vya maelfu ya watu, kuwageuza mamilioni kuwa wakimbizi na kuidumbukiza nchi hiyo kwenye mgogoro mbaya zaidi wa kibinadamu duniani.

Hata hivyo, licha ya juhudi mbalimbali za kuvimaliza vita nchini Sudan bado imeshuhudiwa mara kadhaa jitihada hizo zikishindwa kuzaa matunda.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW