1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Janga

Ubelgiji yakumbuka miaka 10 ya shambulio la kigaidi

22 Machi 2026

Ubelgiji leo (22.03.2026), imewakumbuka watu waliouwawa katika shambulio la kigaidi miaka 10 iliyopita lililotokea Machi 22, 2016.

Belgien Brüssel 2026 | Kumbukizi ya miaka 10 ya shambulio la kigaidi
Ubelgiji yakumbuka miaka 10 ya shambulio la kigaidiPicha: Nicolas Maeterlinck/Belga/AFP

Wafanyakazi na timu ya waokoaji walikusanyika katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Brussels wakishikana mikono wakiunda laini ndefu kabla ya bao la ukumbusho kufunguliwa na mfalme Philippe na waziri Mkuu wa Ubelgiji Bart De Wever.

Muda mfupi baadae misa ya kuwakumbuka walioaga dunia ikafanyika katika kituo cha treni za chini za Maelbeek.

Mashambulizi hayo yanadaiwa kufanywa na watu watatu wakujitolea muhanga kutoka  kundi la dola la kiislamu IS, waliojiripua katika uwanja huo wa ndege na katika kituo hicho cha treni.

Watu 36 waliuwawa na wengine 340 walijeruhiwa. Katika kumbukizi hiyo Waziri Mkuu De Wever aliishukuru timu ya kutoa huduma za dharura kwa kuwasaidia watu haraka na kuwahimiza kutokata tamaa.

Amesema siku zote Ugaidi unatumika kuwagawa watu na kuwatia hofu, lakini miaka 10 baadae kinachoonekana ni mshikamano, ubinaadamu na utu.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW