1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchumi wa dunia uko katika "tishio kubwa": Mkuu wa IEA

23 Machi 2026

Mkuu wa Shirika la Nishati la Kimataifa - IEA Fatih Birol amesema kwamba uchumi wa dunia uko chini ya "tishio kubwa" kutokana na mgogoro wa nishati unaosababishwa na vita vya Mashariki ya Kati.

Mkuu wa IEA - Fatih Birol
Mkuu wa Shirika la Nishati la Kimataifa - IEA Fatih Birol ameonya hakuna nchi itakayokwepa athari za mgogoro wa nishati.Picha: Ludovic Marin/AFP/Getty Images

Akizungumza katika hafla ya Waandishi wa Habari katika mji mkuu wa Australia, Birol aliulinganisha mgogoro wa sasa wa nishati na ule wa miaka ya 1970 na athari za uvamizi wa Urusi dhidi ya Ukraine mwaka wa 2022. Mkuu huyo wa IEA amesema kiasi ya vituo arobaini vya nishati vimeharibiwa kwa kiasi kikubwa katika Mashariki ya Kati kutokana na vita katika eneo hilo.

Amesema mambo yalivyo sasa ni kuwa kuna migogoro miwili ya mafuta na mmoja wa gesi, ambayo imeunganishwa pamoja. Birol amesema anatumai kuwa hali hiyo itatuliwa haraka iwezekanavyo akiongeza kuwa IEA inashauriana na serikali za Asia na Ulaya kuhusu kutolewa kwa mafuta ya akiba kama itahitajika. Mataifa wanachama wa IEA walikubaliana Machi 11 kutoa mapipa milioni 400 ya mafuta kutoka kwenye hifadhi za kimkakati ili kupambana na kupanda kwa bei za mafuta ghafi duniani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW