1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchunguzi kuhusu mauaji ya halaiki Rwanda kuanzishwa tena

21 Juni 2023

Mahakama ya rufaa ya mjini Paris, Ufaransa, imetoa agizo la kuanzishwa tena uchunguzi kuhusu madai ya kushindwa kwa jeshi la Ufaransa kuingilia mauaji ya halaiki yaliyotokea wakati wa vita vya mwaka 1994 nchini Rwanda.

Hutus begrüßen französische Soldaten
Picha: dpa/picture alliance

Vyanzo kadhaa vimeliambia shirika la habari la AFP kwamba uamuzi huo umekuja baada ya wachunguzi mwaka jana kuifunga kesi hiyo.

Mashirika kadhaa na watu walionusurika mauaji ya Kimbari nchini Rwanda yaliyofanywa dhidi ya jamii ya Watutsi, katika milima ya Bisesero, magharibi mwa Rwanda, kwa muda mrefu wamekuwa wakiutuhumu ujumbe maalum  wa jeshi la Ufaransa na serikali kuwa washirika wa mauaji hayo,wakisema wanajeshi hao walifanya makusudi kushindwa kuwalinda wahanga kwa siku tatu wakati mauaji yakiendelea.

Mamia ya Watutsi waliuwawa katika eneo hilo la milima ya Bisesero kati ya Juni 27 na 30 mwaka 1994.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW