1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Ufaransa kuifunza Ukraine kutumia ndege za kivita za Mirage

8 Juni 2024

Rais Emmanuel Macron amesema Ufaransa inapanga kuanza mara moja kuwafunza marubani na mafundi wa Ukraine namna ya kuziendesha ndege za kivita aina ya Mirage, ambazo imeahidi kuzipeleka Kyiv.

Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa
Rais Emmanuel Macron asema Ufaransa itaanza mara moja kuwafundisha marubani wa Ukraine namna ya kutumia ndege za kijeshi za Mirage itakazozipeleka KyivPicha: Jana Rodenbusch/Pool Photo /picture alliance

Macron Amesema hayo baada ya mazungumzo na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky katika makazi ya rais ya Élysée jijini Paris.

Macron hata hivyo bado hajaainisha idadi ya ndege ambazo Ufaransa na mataifa mengine wanataraji kuzipeleka Ukraine ambayo inapambana na Urusi.

Soma pia: Macron na Scholz wazungumzia mzozo wa Ukraine

Ufaransa bado inahitaji kuhitimisha mchakato huo kwa kuamua juu ya idadi ya ndege itakayopeleka pamoja na mazungumzo ya mpango wa pamoja ulioanza miezi kadhaa iliyopita na mataifa washirika.

Rais Volodymyr Zelensky amemshukuru Macron kwa ahadi hiyo ya kupeka ndege hizo za kijeshi za Mirage ili kusaidia juhudi za Kyiv za kulinda anga zake dhidi ya mashambulizi ya Urusi.

Rais Emmanuel Macron akiwa na Rais wa ukraine Volodymyr Zelensky pamoja na wake zao nchini Ufaransa. Zelensky alikwenda Ufaransa kwenye maadhimisho ya miaka 80 ya D-DayPicha: Ludovic Marin/Pool via REUTERS

Ukraine yaishukuru Ulaya, katikati ya hofu dhidi ya mashambulizi makali ya Urusi

"Ndege zenu, mheshimiwa.. ndege za kivita, zinazoendeshwa na marubani wa Ukraine zinadhihirisha uthabiti wa Ulaya, kwamba Ulaya ni thabiti kuliko uovu," alisema Zelensky siku ya Ijumaa katika hotuba yake kwenye bunge la Ufaransa, mjini Paris.

Soma pia: Zelensky aisihi Ulaya kutochoka kuisadia Ukraine

"Ufaransa inapanga kuanza mara moja kuwafundisha marubani na mafundi kuhusiana na uendeshwaji wa ndege hizo. Hili litaanza hapa ufaransa katika siku chache zijazo," alisema Macron katika kasri la rais la Élysée.

Macron alitangaza pia msaada wa dola milioni 200 kwa ajili ya kuisaidia Ukraine kiuchumi na hususan makampuni, yanayotaka kuwekeza kwenye miundombinu iliyoharibiwa vibaya na mashambulizi.

Soma pia: Marekani kupeleka Ukraine msaada mpya wa kijeshi wa dola mil. 225

Zelensky aidha amewaambia wabunge wa ufaransa mapema siku ya Ijumaa kwamba Rais wa Urusi Vladimir Putin ni "mpinzani wa Ulaya" na hataumaliza uvamizi wake nchini Ukraine, akiifananisha kampeni ya Moscow na ile ya Adolf Hitler wakati wa Vita vya Pili vya dunia.

"Mazingira yanafanana na ya sasa, kama ya miaka ya 1930, wakati Hitler alipokuwa akifanya hivihivi dhidi ya majirani yake," alisema Zelensky.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW