1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa, Ujerumani kuipa msaada wa ulinzi wa anga Ukraine

29 Agosti 2025

Ufaransa na Ujerumani zimeahidi kuipa Ukraine vifaa zaidi vya ulinzi wa anga. Nchi hizo mbili zimetoa ahadi hiyo baada Urusi kufanya mashambulizi makubwa ya anga dhidi ya nchi hiyo katika siku za karibuni.

Touloun, Ufaransa 29.08.2025
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz Picha: Manon Cruz/REUTERS

Katika taarifa ya pamoja nchi hizo zimesema licha ya juhudi kubwa za kidiplomasia, Urusi haijaonesha nia ya kuvimaliza vita dhidi ya Ukraine. Ahadi ya nchi hizo mbili kwa umoja wa Ulaya imetolewa wakati wa mutano wao wa pamoja uliowakutanisha Rais Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz huko Touloun Ufaransa. Nchi hizo zimeahidiana pia kuboresha zaidi ushirikiano wao katika masuala ya usalama. Hayo yanajiri wakati mawaziri wa ulinzi na mambo ya nje wa Umoja wa Ulaya wakiwa mjini Copenhagen kujadili namna ya kuiunga mkono zaidi Ukraine iliyo vitani na Urusi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW