1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAustralia

Ufilipino na Australia zasaini makubaliano ya ushirikiano

8 Septemba 2023

Ufilipino na Australia zimeimarisha muungano wao wa kiusalama na kiuchumi kwa kutia saini ushirikiano wa kimkakati mnamo wakati zikitafuta njia za kukabiliana na ushawishi unaokuwa wa China katika kanda hiyo.

Philippinen | Besuch Anthony Albanese in Manila
Picha: Earvin Perias/REUTERS

Makubaliano hayo yalikamilishwa baada ya mkutano kati ya rais wa Ufilipino Ferdinand Marcos na waziri mkuu wa Australia Anthony Albanese  aliekuwa ziarani mjini Manila.

Ziara ya Albanese iliyokuwa mwanzo wa mazungumzo ya pande mbili kati ya nchi hizo mbili ndani ya miaka 20, ilijiri baada ya misururu ya mikutano ya maafisa wa ngazi za serikali yake kuzuru Ufilipino tangu Marcos alipochukua madaraka mwaka 2022.

Chini ya ushirikiano huo wa kimkakati, nchi hizo zitapania kutanua ushirikiano wao katika Nyanja za ulinzi, usalama, tabia nchi na elimu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW