Ufilipino yakosoa mazoezi ya kijeshi ya China Taiwan
31 Desemba 2025
Matangazo
Waziri wake Gilberto Teodoro amesema hali inayoshuhudiwa inaendelea "kutanua ufa" katika eneo ambalo tayari ni tete na athari zake zinaweza kutanuka zaidi na kulemaza yaliyopwaya, miongoni mataifa jirani na mlango bahari wa Taiwan na kanda nzima ya bahari ya Hindi na Pasifiki.
China kwa upande wake imepuzilia mbali nchi yoyote inayokosoa mazoezi yake ya kijeshi ikiwemo Japan, Australia na baadhi ya nchi za Ulaya ikisema ukosoaji huo "hauna msing".
China ilianzisha mazoezi hayo ya kijeshi siku ya Jumatatu yanayojumuisha meli za kivita, wapiganaji, makombora na madroni. Mazoezi hayo yanalenga kuonesha utayari wa kukabiliana kupitia majini, kukizingira kisiwa hicho hasa katika bandari na maeneo yake muhimu.