1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uhispania yanyakua ubingwa wa EURO 2024

15 Julai 2024

Uhispania ndio mfalme mpya wa soka barani Ulaya baada ya kupata ubingwa kwa kupiga England bao 2-1 katika fainali iliyopigwa usiku wa Julai 14, 2024 mjini Berlin.

Ujerumani Berlin |Fainali za UEFA EURO 2024 | Uhispania yashinda EURO 2024
Wachezaji wa Uhispania wakishangalia ubingwa wa EURO 2024 baada ya fainali zilizofanyika mjini Berlin Julai 14, 2024. Picha: Wolfgang Rattay/REUTERS

Kocha wa timu ya taifa ya Uhispania Luis de la Fuente amewashukuru wachezaji wake kwa kuweka rekodi ya kushinda taji lao la nne la mashindano ya soka ya Ulaya ya Euro.

De la Fuente aliirithi nafasi ya Luis Enrique baada ya timu ya Uhispania kuondolewa katika Kombe la dunia la mwaka 2016 kwenye duru ya mtoano ya 16 bora huku wengi wakikosa matumaini kwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 63.

Baada ya kushindwa na Scotland katika mechi za kuwania kufuzu mashindano ya Euro mnamo mwezi Machi mwaka jana, baadhi ya vyombo vya habari vilisema kwamba ataachishwa kazi.

Lakini  timu hiyo iilijipanga vyema na haijashindwa tangu wakati huo na sasa ni mabingwa wapya wa soka, Ulaya mwaka 2024.

Ruka sehemu inayofuata Gundua zaidi
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW