1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uholanzi, Ubelgiji zajiunga kwenye uchunguzi kuhusu Wayazidi

26 Juni 2023

Uholanzi na ubelgiji zimejiunga kwenye uchunguzi wa Kimataifa kuhusu vitendo vya mauaji vilivyofanywa dhidi ya jamii ya wachache ya Wayazidi katika nchi za Syria na Iraq.

Irak 2 Jahrzehnte nach Saddams Sturz | Suche nach Vermissten
Picha: THAIER AL-SUDANI/REUTERS

Timu ya pamoja ya uchunguzi, ilianzishwa na Ufaransa na Sweden Oktoba mwaka 2021 na kuungwa mkono na shirika la Eurojust lenye makao yake mjini The Hague, Uholanzi kwa lengo la kuwafungulia mashtaka wafuasi wa itikadi kali kutoka nchi za kigeni, waliowalenga jamii ya Wayazidi wakati wa vita katika nchi za Syria na Iraq.

 Tayari tumu hiyo imefanikiwa kuwatambuwa watu wawili raia wa Ufaransa, mtu na mkewe wafuasi wa itikadi kali, waliohusika kwa mauaji ya mtu wa  jamii ya Yazidi.

Timu hiyo ya uchunguzi wa pamoja ni sehemu ya juhudi pana za kimataifa za kutafuta haki kuhusu mauaji yaliyowalenga Wayazidi, waliolengwa na kundi linalojiita Dola la Kiislamu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW