1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uingereza na Rwanda mahakamani juu ya mkataba wa wahamiaji

18 Machi 2026

Uingereza na Rwanda zitakutana katika Mahakama ya Kudumu ya Usuluhishi (PCA) huko The Hague kuanzia leo Jumatano, huku Kigali ikidai zaidi ya pauni milioni 100 kutoka kwa Uingereza .

Uhamiaji
Wahamiaji wanaojaribu kuvuka ujia wa bahari ya Atlantiki, waokolewa mnamo Juni 15, 2022Picha: Ben Stansall/AFP

Maafisa kutoka nchi hizo mbili watawasilisha kesi yao katika kikao cha siku tatu mbele ya mahakama hiyo ya kimataifa iliyoanzishwa mwaka 1899 kusuluhisha mizozo ya kimkataba kati ya mataifa.

Maafisa kutoka Rwanda watawasilisha kesi yao leo Jumatano, huku mawakili wa Uingereza wakijibu kesho Alhamisi. Pande zote mbili zitahitimisha uwasilishaji wao siku ya Ijumaa.

Jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo ya PCA litasimamia kesi hiyo na huenda likachukuwa miezi kadhaa kutoa uamuzi.

Tayari mataifa hayo mawili yako kwenye mvutano baada ya Uingereza kupunguza misaada kwa Rwanda, ikiituhumu kuwaunga mkono waasi wa M23 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW