1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani haiwezi tena kushirikiana na Niger kijeshi

17 Julai 2024

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Annalena Baerbock amesema Ujerumani haiwezi tena kushirikiana kijeshi na Niger kwa sababu ya ukosefu wa "imani" katika uhusiano na utawala wa kijeshi wa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Annalena Baerbock
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Annalena BaerbockPicha: dts-Agentur/picture alliance

Akizungumza katika mkutano wa pamoja na Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara, Baerbock amesema licha ya ushirikiano kati ya mataifa hayo kuharibika, bado Ujerumani haija sitisha misaada ya kibinadamu kwa sababu watu wa Niger hawahusiki na kile kilichotokea.

Ujerumani mnamo Julai 6 ilitangaza kwamba itamaliza operesheni kwenye kituo chake cha anga nchini Niger na kuwaondoa wanajeshi wake dazeni tatu waliosalia ifikapo Agosti 31.

Baerbock afanya ziara Afrika Magharibi

Niger imekuwa ikiongozwa na utawala wa kijeshi tangu mapinduzi ya Julai 2023 yaliyomuondoa madarakani Rais Mohamed Bazoum, ambaye amekuwa akishikiliwa kama mfungwa tangu wakati huo.
 
Aidha utawala huo umewapa kisogo washirika wengine wa Magharibi kama vile Ufaransa na Marekani na kuegemea upande wa Urusi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW