1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani kupendekeza hatua ya kuwasajili vijana jeshini

12 Juni 2024

Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius anatarajiwa kuwasilisha pendekezo la kuwataka vijana wote wa kiume kujisajili jeshini.

Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius
Waziri wa ulinzi wa Ujerumani Boris PistoriusPicha: Christoph Hardt/Panama Pictures/picture alliance

Haya ni kulingana na shirika la habari la Ujerumani, DPA. Hatua hii ya Pistorius inakuja miaka 13 baada ya Ujerumani kufutilia mbali sharti la vijana kusajiliwa jeshini.

Shirika la habari la DPA linaeleza kwamba pendekezo hilo la Pistorius halitorudisha hatua hiyo ya vijana kusajiliwa kwa mafunzo ya jeshi kwa lazima ila watahitajika kutoa taarifa kuhusiana na iwapo wako tayari kuhudumu jeshini kwa hiari.

Waziri huyo wa ulinzi wa Ujerumani atabainisha yote yaliyoko kwenye mpango wake Jumatano 12.06.2024. Ingawa Ujerumani ilifutilia mbali sheria hiyo ya vijana kulazimishwa kujisajili jeshini, sheria iliyopo bado inatoa uwezekano wa hilo kufanyika endapo kuna vita au mivutano mingine.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW