1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUjerumani

Ujerumani: Mchakato wa amani Gaza utakuwa mgumu

1 Oktoba 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul amesema taifa hilo liko tayari kusaidia utekelezwaji wa pendekezo la mpango wa amani wa Gaza ulioratibiwa na Rais Donald Trump wa Marekani.

Ujerumani 2025 | Waziri wa Mambo ya Nje Johann Wadephul akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kabla ya kuondoka kuelekea kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Wolfgang Wadephul (CDU), Waziri wa Mambo ya Nje, akizungumza na vyombo vya habari kabla ya kuhudhuria Mkutano wa 80 wa baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New YorkPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Hata hivyo Wadephul ambaye alizungumza na shirika la habari la Funke na matamshi yake kuchapishwa,  amesema huenda usianze kutekelezwa mara moja.

Waziri huyo amesema kwamba bado kuna maswali mengi magumu kuhusiana na namna mpango huo utakavyotekelezeka, ikiwa ni pamoja na namna Gaza itakavyotawalika, hakikisho la usalama na hata namna misaada ya kiutu itakavyorejeshwa Gaza na kusisitiza kwamba utakuwa ni mchakato mgumu.

Alipozungumza na kituo cha utangazaji cha ZDF jana Jumanne alisema pia kuna mashaka ikiwa mataifa ya Kiarabu na kundi la Hamas watakubaliana nao na kuongeza kuwa atakwenda Qatar siku ya Jumapili akisistiza kuitumia vyema fursa hii kumaliza mateso dhidi ya watu wa pande zote mbili.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW