1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uamuzi wa kuchunguza ruzuku za China wapongezwa

13 Septemba 2023

Ufaransa na Ujerumani zimeukaribisha uamuzi wa Umoja wa Ulaya kuanzisha uchunguzi dhidi ya ruzuku zinazotolewa na serikali ya China kwa makampuni ya magari ya umeme.

Hongkong | 25. Jahrestag der Rückgabe an China
Picha: Magnum Chan/AP Photo/picture alliance

Ufaransa imesema Jumuiya hiyo inapaswa kutetea maslahi yake.

Waziri wa fedha wa Ufaransa Bruno Le Maire ameuambia mkutano wa waandishi habari  mjini Berlin,muda mfupi baada ya rais wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya,Ursula von der Leyen kutangaza hatua hiyo,mbele ya bunge la Ulaya,mjini Strassburg,kwamba kuanzishwa kwa uchunguzi huo ni uamuzi mzuri sana.

Ujerumani kupitia waziri wake wa uchumi, Robert Habeck imesema uchunguzi dhidi ya ruzuku inayotolewa na serikali ya China,unaonesha mwelekeo mzuri wa Umoja wa Ulaya na unahusu zaidi kutafuta suluhu ya ushindani usiokuwa wa haki.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW