1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani yaonya kupanuka kwa mgogoro Mashariki ya Kati

18 Machi 2026

Ujerumani na Ufaransa zimetoa wito wa kukomeshwa kwa vita Mashariki ya Kati huku mwanadiplomasia mkuu wa Ujerumani Johann Wadephul akionya kuhusu "mgogoro wa hali mbaya zaidi" ikiwa usambazaji bidhaa duniani utavurugika.

Ubelgiji Brüssel 2026 | Johann Wadephul
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul akizungumza na waandishi wa habari mjini Brussels mnamo Machi 16, 2026Picha: Nicolas Tucat/AFP/Getty Images

Wadephul amesema 'mashambulizi yasiyo ya msingi kabisa, yanayoyalenga mataifa ya Ghuba kwa sasa pia yanaonyesha kwamba kuna uwezekano wa vita kuongezeka.

''hali inaweza kulitumbukiza sio eneo hili la Mashariki ya Kati bali ulimwengu mzima unaweza kutumbukia katika mgogoro mkubwa na mbaya zaidi.''

Wadephul ameongeza kusema kuwa lazima wajaribu kutafuta namna ambayo malengo ya kijeshi ya Marekani na Israel yanaweza kufikiwa ili kupunguza mapigano na kukomesha uhasama.

Akiwa pamoja na Wadephul mjini Berlin, waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot pia alitoa wito wa kusitishwa haraka kwa vita na kukomeshwa kwa uhasama.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW