1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ukraine kuwaomba washirika wake ufadhili wa dola bilioni 20

12 Juni 2026

Ukraine itatafuta dola bilioni 20 za ziada za ufadhili wa kijeshi kutoka kwa washirika wake katika mkutano utakaofanyika wiki ijayo.

Uhispania, Madrid 2026 | Volodymyr Zelensky katika mkutano na waandishi wa habari huko palacio de la Moncloa mnamo Machi 18, 2026
Rais wa Ukraine Volodymyr ZelenskyPicha: Javier Soriano/AFP

Ombi hilo litawasilishwa Alhamisi ijayo katika mkutano wa Kundi la Msaada wa Ulinzi kwa Ukraine, muungano wa zaidi ya nchi 50 unaojulikana pia kama Kundi la Ramstein, ambapo washirika hupanga na kuratibu msaada wa kifedha na kijeshi kwa Ukraine .

Kwa mujibu wa chanzo hicho, baadhi ya washirika wataombwa kuchangia kati ya dola bilioni 2 hadi 6 kila mmoja ili kufikia lengo la dola bilioni 20, ama kwa mfumo wa misaada au mikopo.

Wakati huo huo, jeshi la  Ukraine lilisema leo kuwa limefanya mashambulizi ya usiku kucha dhidi ya viwanda viwili vya kusafisha mafuta katika eneo la Tatarstan nchini Urusi.

Makao Makuu ya Jeshi hilo yameeleza kuwa mashambulizi hayo ni sehemu ya operesheni zake za kulenga miundombinu ya nishati inayosaidia juhudi za kijeshi za  Urusi katika vita vinavyoendelea kati ya nchi hizo mbili.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW