SiasaUkraine
Ukraine: Urusi inaishikilia Belarus kama mateka wa nyuklia
26 Machi 2023![Ukraine Kiew | Sekretär des Nationalen Sicherheits- und Verteidigungsrats der Ukraine Oleksij Danilow](https://static.dw.com/image/64636503_800.webp)
Matangazo
Kauli hiyo imetolewa na Katibu wa Baraza la Usalama na Ulinzi la Kitaifa la Ukraine, Oleksiy Danilov, kupitia ukurasa wake katika mtandao wa kijamii wa Twitter, akiongeza kuwa hiyo ni "hatua ya kudhoofisha utulivu wa ndani wa nchi hiyo".
Shirika la habari la Tass lilimnukuu Rais Vladimir Putin akisema kuwa Urusi ilifikia makubaliano na jirani yake Belarus ili kupeleka silaha za kimkakati za nyuklia.
Soma pia: Viongozi wa Ulaya kuharakisha kuipatia Ukraine silaha
Hata hivyo, Idara ya Ulinzi ya Marekani imesema hakuna dalili zozote kwamba Urusi inajiandaa kutumia silaha za nyuklia baada ya tangazo hilo.