1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Ukraine, Urusi zaripoti vifo baada ya kushambuliana

21 Januari 2026

Ukraine na Urusi zimeripoti kutokea vifo kufuatia mashambulizi ya kila upande dhidi ya mwengine kwenye makabiliano ya usiku wa kuamkia Jumatano (Januari 21).

Ukraine Zaporizhzhia 2026
Wanajeshi wa Ukraine wakijitayarisha kufanya mashambulizi kwenye mkoa wa Zaporizhzhia mwanzoni mwa mwezi Januari 2026.Picha: Andriy Andriyenko/Ukraine's 65th Mechanized Brigade/AP Photo/picture alliance

Raia watatu wametajwa kuuawa kwa mashambulizi ya Urusi katika mji wa kusini mashariki wa Zaporizhzhia nchini Ukraine, kwa mujibu wa Gavana Ivan Fedorov, ambaye alisema mashambulizi hayo yamesababisha pia kukatika kwa umeme kwenye mkoa wake.

Kwa upande wa Urusi, gavana wa mkoa wa Belgorod, ameripoti kifo cha afisa mmoja wa usalama, huku vifo vyengine viwili vikiripotiwa kwenye mkoa wa Bryansk.

Kwengineko, watu wanane wamejeruhiwa kufuatia mripuko katika mji wa Urusi wa Adygea, mashariki mwa Bahari Nyeusi.

Ni nadra kwa Ukraine, ambayo imekuwa ikikabiliana na uvamizi wa Urusi kwa takribani miaka minne sasa, kufanya mashambulizi ndani ya ardhi ya Urusi kutokana na kulemewa kivita.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW