SiasaUkraine
Ukraine yaishutumu Urusi kuwashambulia raia
10 Machi 2023![Ukraine Kiew Luftangriffe durch Russland](https://static.dw.com/image/64941640_800.webp)
Matangazo
Zelensky amesema mashambulizi makubwa ya anga mapema jana ni jaribio jengine la serikali ya kigaidi kupigana vita dhidi ya ustaarabu.
Ukraine imesema takribani raia tisa waliuawa wakati wa mashambulizi, yaliyohusisha makombora yaliyorushwa Kiev na kusababisha umeme kukatika katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo. Maafisa wa Ukraine wamesema watu waliouawa walikuwa wanavijiji katika jimbo la Lviv, karibu na mji wa eneo la mapambano wa Dnieper na mji wa Kharkiv.
Aidha, jeshi la Ukraine limesema limedungua ndege nyingi zisizo na rubani pamoja na makombora wakati wa mashambulizi yaliyofanyika ndani ya mwezi mmoja. hata hivyo, Urusi imeendelea kukanusha madai ya kuwalenga raia katika vita vyake Ukraine.