1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaHungary

Ukraine yaituhumu Hungary kwa utekaji

6 Machi 2026

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Adrii Sybiha, ameituhumu Hungary kwa kuwateka nyara wafanyakazi wa benki wa Ukraine waliokuwa wakisafirisha dola milioni 40 na kilo tisa za dhahabu mapema leo.

Ubelgiji Brüssel 2025 | Andriy Sybiha
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andriy Sybiha, anasema Hungary 'imewateka nyara' wafanyakazi wa benki ya nchi yake wakiwa na dola milioni 40 taslimu.Picha: Nicolas Tucat/AFP/Getty Images

Sybiha ameandika kwenye mtandao wa X kwamba raia saba wa Ukraine wanaofanya kazi na benki ya serikali, Oschadbank, walitekwa mjini Budapest wakati wakiwa na magari ya benki hiyo yanayosafirisha fedha kutokea Austria.

Benki hiyo imethibitisha kukamatwa kwa wafanyakazi hao. Sybiha ameituhumu Hungary kwa kile alichokiita utekaji nyara na wizi wa fedha.

Hakukuwa na majibu ya mara moja kutoka serikali ya Hungary kufuatia tuhuma hizo za Ukraine.

Hungary ni mojawapo ya mataifa machache ya Ulaya yanayoendelea kuwa na uhusiano mzuri na Urusi tangu uvamizi wake dhidi ya Ukraine na imekuwa daima ikipinga msaada wa kijeshi kwa Kiev. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW