1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Ukraine yamteua Fedorov kuwa waziri wa ulinzi

14 Januari 2026

Ukraine imemteua waziri wake wa nne wa ulinzi katika kipindi cha karibu miaka minne tangu ilipovamiwa kikamilifu na taifa jirani la Urusi.

Ukraine Kyiv 2025 | Majadiliano kuhusu akili bandia kwa ajili ya kushtaki uhalifu wa kivita wa Urusi
Mykhailo Fedorov, Waziri wa Mabadiliko ya Kidijitali wa Ukraine anahudhuria mjadala kuhusu jukumu la akili bandia katika kulifikisha Shirikisho la Urusi mbele ya sheria kwa ajili ya vita nchini Ukraine.Picha: Pavlo Bahmut/Ukrinform/Photoshot/picture alliance

Hatua hiyo ilifikiwa baada ya wabunge 277 kumpigia kura Mykhailo Fedorov kushika wadhifa huo, katika jaribio la pili baada ya kura ya awali kukwama kwa kukosekana kwa wabunge wa kutosha.

Rais Volodymyr Zelensky alikuwa tayari amemteua Fedorov ambaye anatimiza miaka 35 wiki ijayo. Amekuwa waziri wa mageuzi ya kidijitali tangu mwaka 2019 na alisimamia upanuzi wa uzalishaji wa droni baada ya uvamizi wa Urusi mwaka 2022

Wakati huo huo, aliyekuwa waziri wa ulinzi Denys Shmyhal ameteuliwa kuwa waziri wa nishati na naibu waziri mkuu wa kwanza, siku chache baada ya kuondolewa kwenye wizara ya ulinzi, aliyoiongoza kwa chini ya miezi sita.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW