Ukraine yaripoti mashambulizi mapya mjini Kiev
9 Machi 2023![Ukraine Krieg | Russische Raketen in Charkiw](https://static.dw.com/image/64926643_800.webp)
Matangazo
Katika ujumbe kupitia mtandao wa Telegram, meya wa Kiev Vitali Klitschko, amethibitisha kuwa wilaya ya Kusini mwa Kiev, Holosiiv ililengwa na kuongeza kuwa karibu asilimia 15 ya makazi mjini humo kwasasa hayana umeme.
Wagner lasema jeshi la Urusi limezinyakua wilaya kadhaa Ukraine
Mashambulizi ya makombora ya Urusi yanayolenga miundo mbinu ya nishati, pia yamesababisha ukosefu wa umeme katika eneo la Kusini la Odessa nchini humo pamoja na Kharkiv, katika eneo la Mashariki, kwa mujibu wa maafisa katika maeneo hayo.
Kupitia mtandao wa Telegram, gavana wa kijeshi wa Odessa Maksym Marchenko, amesema kutokana na mashambulizi hayo makubwa, kituo kimoja cha nishati cha kikanda kililengwa na jumba la makazi kuharibiwa.