SiasaUkraine
Ukraine yasema bado yaudhibiti mji wa Bakhmut
23 Mei 2023Matangazo
Bi Maliar ameandika katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii wa Telegram kuwa vikosi vya Kyiv vimepiga hatua fulani eneo la kaskazini na kusini mwa Bakhmut na kwamba vikosi vya Urusi, ambavyo vinadai kuunyakua mji huo, vimeendelea tu kujiimarisha kwenye maeneo wanayoyadhibiti.
Soma pia; Yanayojiri Ukraine: Mashambulizi yaripotiwa Belgorod
Urusi imesema imeanzisha uchunguzi kuhusu vitendo vya kigaidi baada ya shambulio la kuvuka mpaka hapo jana katika eneo lake la Belgorod na kuyashutumu makundi yenye silaha ya Ukraine kuhusika na shambulio hilo. Tuhma zinazokanushwa na Kiev.