Ukraine yasema Urusi imeishambulia meli ya mizigo ya kiraia
5 Machi 2026
Matangazo
Mashambulizi hayo yamefanyika usiku wa kuamkia Alhamis.
Kulingana na gavana wa kijeshi wa Odesa Oleg Kiper, mabaharia kadhaa wamejeruhiwa katika shambulizi hilo.
Kiper ambaye hakutoa idadi ya waliojeruhiwa amesema kuwa meli hiyo ilikuwa inasafirisha mahindi. Urusi ambayo imepinga kuwalenga raia, imetahadharisha kuwa meli yoyote inayoelekea katika bandari za Ukraine, itachukuliwa kama inayobeba mizigo ya kijeshi.
Haya yanafanyika wakati ambapo angalau watu watano wamejruhiwa katika mashambulizi mawili ya Urusi yanayolenga miundo mbinu ya reli kusini mwa Ukraine.
Kulingana na maafisa wa Ukraine, mfanyakazi wa reli alijeruhiwa baada ya droni kuipiga treni ambayo ilikuwa haina abiria mwendo wa asubuhi katika eneo la Mykolaiv.